MGANGA WA DIOMOND AFUNGUKA: Diamond ANAENDA NJE YA MAAGANO YETU, Anguko lake laja.



Anayedaiwa kuwa ni mganga wa zamani wa Diamond, Dktari. Shehe. Yahaya amefunguka na kusema kuwa Diamond amekiuka masharti aliyompa na kuwa watu wategemee kuanguka kwake siku yoyote..

Ametiririkaaa... "Ilikuwa awe msaada kwa wengine/wasanii wachanga, anasa zimeniudhi na ilikuwa nje ya makubaliano yetu pia ni kinyume na masharti ya dawa niliyompa inayoitwa SALALA".

Alisema kuwa wasanii kama Belle 9 na Ali Kiba ndo walikuwa hit kipindi kile cha KAMWAMBIE lakini waliwazima kwa kumpa nyota hiyo Diamond. Alisisitiza kuwa kuna maagano mengi ambayo hata hayastahili kusemwa ameshindwa kuyatimiza na akimpigia simu anamuona kama adui.

Ustadh na Daktari huyo aliongeza kuwa mwanzo Diamond alikuwa anakuja kwa miguu na hata kuishia kula nyumbani kwake lakini sasa anamuona kama adui baada ya kuharibu masharti na kusema kuwa muda sio mrefu atashuka kabisa kimuziki hata yeye anajua.

Shehe, Yahaya alisisitiza kuwa hata wakikutanishwa hatasita kuongea na kuwa ataona aibu tuu, pia kuhusu Free mason alisema kuwa Diamond hayupo huko na ni uvumi anayeueneza yeye mwenyewe lakini anguko lake laja, Shehe alitaja namba yake kwa yeyote atakayetaka maelezo zaidi kuhusu hili: 0714 866416.

Vumilia - Dushe Dushe [Official Video]


RECHO - Nashukuru Umerudi Video


WALTER KUKINUKISHA DODOMA

 Baada ya kushindaMil. 50 za Epiq BSS 2012 Walter Chilambo atazunguka na washiriki wengine sita (6) wa shindano hilo mwaka jana kukinukisha Dodoma tarehe 15.

Pamoja na burudani yao watasindikizwa na Ben Pol, Barnaba, Ali Nipishe na Lina na hii ni baada ya Walter kuachia ngoma yake mpya Ijumaa hii ya tarehe 8..
Ben Pol ni moja kati ya wanaomkubali Walter pia aliahidi kufanya nae kazi..

TAARIFA YA POLISI MBEYA 05TH FEB. 2013

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 05. 02. 2013.
 
 
WILAYA YA MBEYA MJINI - MAUAJI
 
MNAMO TAREHE 03.02.2013 MAJIRA YA SAA 18:00HRS HUKO KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. AMBOKILE S/O KIKWALE,MIAKA 16,MNYIHA,MKULIMA MKAZI WA ILEMI ALIFARIKI DUNIA WAKATI AKIENDELEA KUPATIWA MATIBABU HOSPITALINI HAPO BAADA YA KUPIGWA KWA KUTUMIA FIMBO NGUMI NA MATEKE NA MAMA YAKE MDOGO [MAMA WA KAMBO ]  BUPE W/O JOSEPH KIKWALE,KYUSA,MIAKA 32,MKULIMA MKAZI WA ILEMI  MAJIRA YA SAA 17:00HRS .CHANZO NI MTUHUMIWA KUMTUHUMU MAREHEMU KUWA ANAMUIBIA PESA NYUMBANI KWAKE  ENEO LA ISANGA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA HOSPITALINI HAPO. MTUHUMIWA AMEKAMATWA NA TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAFANYWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI NA BADALA YAKE WATATUE MATATIZO YA KIFAMILIA KWA NJIA YA MAZUNGUMZO ILI KUEPUSHA MATATIZO YANAYOWEZA KUEPUKIKA.
 
 
WILAYA YA RUNGWE - AJALI YA GARI NA KUSABABISHA KIFO
 
MNAMO TAREHE 02.02.2013 MAJIRA YA SAA 19:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA LWANGWA WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA. IPYANA S/O SILWIMI,MIAKA 36,KYUSA ,DEREVA MKAZI WA KIJIJI CHA KIKOTA ALIRUKA KUTOKA KWENYE GARI T.482 AYB AINA YA ISUZU ALILOKUWA AKIENDESHA KISHA GARI HILO KUMKANYAGA . MAREHEMU ALIFARIKI DUNIA MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA KATIKA HOSPITALI YA MISHENI ITETE KWA MATIBABU. CHANZO CHA AJALI NI GARI KUSHINDWA KUPANDA MLIMA NA KURUDI NYUMA AMBAPO DEREVA ALIAMUA KURUKA  NA GARI KUMKANYAGA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANAENDELEA KUTOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI KWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI NA KUWA NA TAHADHARI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO ILI KUEPUSHA MADHARA YANAYOWEZA KUJITOKEZA.
 
 
WILAYA YA CHUNYA - KUPATIKANA NA BHANGI.
 
MNAO TAREHE 03.02.2013 MAJIRA YA SAA 11:30HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA MBANGALA WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA FRENK S/O HAMISI,MIAKA 25,MKULIMA,MNYIHA,MKAZI WA KIJIJI CHA CHANG’OMBE AKIWA NA BHANGI KETE 44 SAWA NA GRAM 220  . MTUHUMIWA NI MUUZAJI NA MVUTAJI WA BHANGI.TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI MTUHUMIWA FAIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANAENDELEA KUTOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.
 
 
 
Signed By,
[DIWANI ATHUMANI – ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA

NU Video: Tillah - Step Out

Tizama video kupitia Infogramme, Bofya katikati kuangalia..

Kioo ambacho Gumzo kitaani DjChoka - Press Play HD feat. B'Hits Artist

BONGO kama MBELE

HotVideo: "PRESS PLAY" - Djchoka ft. B'Hitz Artist

Inawezekana ni kwa sababu huyu jamaa mwenye hii Video (Dj Choka) ni m2 wa mitandao sana, lakini hii ni moja kati ya Video inayoendelea kuangaliwa sana ktk mtandao. Angalia Presds play hapa kwa ku'Press Play hapo kati...

DULLY: Hii ndio gari yangu mpya, Pia sorry kuhusu Arafat Baunsa wangu.. Sijui chochote

Hiki ndicho alichoandika Dully Sykes ktk Website yake kuhusiana na kashfa anayokabiliwa baunsa wake Arafat Ngumi Jiwe,  "Yaani nimeumia sana baada ya kupata taarifa hizi za Arafat Ngumi Jiwe ingawa sijui kama za kweli au laa, lakini mbali na hayo ni habari chafu ambazo zinaweza kunichafua hata mimi kwa sababu huyo ni jamaa yangu wa karibu. Kitendo hicho cha kulawiti mtoto na mimi nikiwa kama baba kinanigusa kwa uchungu sana na kama ni kweli sheria itachukua mkondo wake ili kudhibiti watu wenye tabia hizo chafu".

LULU: Mtetezi wangu MUNGU Pekee, Asanteni WaTanzania mlio nami

LULU: Akiongea na waandishi kwa Huzuni baada ya kukabidhiwa
kwa Mama yake mzazi Leo  baada ya jana masuala kusuasua.
Muda mchche baada ya kukabidhiwa kwa mama yake mzazi, msanii Lulu amesema anawashukuru sana watanzania wanaoendelea kuwa pamoja na yeye na kusema kuwa anamtegemea sana Mwenyezi Mungu kwani yeye ndiye mtetezi wake na kuwa yeye anajua Ukweli kuhusu suala linalomkabili.

LULU Apata Dhamana, Angalia picha 4 na Masharti aliyopewa

Lulu akiwa Mahakamani Leo 28/09/2013

Mahakama kuu leo imetangaza dhamana ya mwigizaji Lulu iwapo atatimiza masharti aliyopangiwa ambayo ni pamoja na kuwasilisha hati yake ya kusafiria, kutosafiri nje ya Dar es salaam, kujiwakilisha au kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila mwezi pamoja na wadhamini wake wawili ambao kila mmoja adhamini kwa shilingi milioni 20 za kitanzania.

Upande wa familia ya Lulu umesema masharti yote yaliyotajwa wanaweza kuyatimiza leo leo hivyo wanasubiri tu jibu la msajili ambae ndio anatakiwa kuhakikisha hayo masharti yametimia kisha ruhusa ya kumkabidhi Lulu kwa familia yake itolewe.

Taarifa za ndani ni kwamba uwezekano wa Lulu kuachiwa upo kuanzia january 29 2013 ambayo ni kesho kwa sababu kuna watumishi wawili wa serikali ambao wapo kikazi mkoani Pwani na ndio walitakiwa kutia saini dhamana ya Lulu wakiwa ni sehemu ya masharti.

Mama mzazi wa Lulu akiwa mahakamani
kusikiliza Dhamana ya mwanaye. (Wa 2 kutoka kushoto)
Lulu akibembelezwa kupigwa picha na mwandishi mmoja wa kike
Lulu akisikiliza Dhamana yake na Masharti aliyopewa..
PICHA zote na MillardAyo.Com

EpiqBSS 2012 Competant Linias Mhaya Introduces 2 U New Song Nanje ndagukunda

Mshiriki wa EBSS 2012 Linias Mhaya ameachia wimbo wake wa kwanza unaitwa Nanje ndagukunda, angalia video hii ya Wimbo huo na Lyrics zake..

KUHUSU DHAMANA YA LULU

Jana kwenye Exclusive on millardayo.com kulikua na stori kwamba uwezekano wa mwigizaji Lulu kuachiwa kwa dhamana january 25 2013 ulikuepo.

Ni kweli ilikua iwe hivyo lakini kwa taarifa  zilizotolewa kwa Millard Ayo ni kwamba dhamana hiyo imeshindikana kutolewa leo.

Sababu kubwa ni leo kuwa sikukuu hivyo shughuli imesogezwa mbele mpaka jumatatu january 28 2013.

Mwanzoni Lulu ambae anatuhumiwa katika kesi ya mauaji bila kukusudia ilidaiwa alikua anatakiwa apate dhamana ambayo milioni 20 zilihitajika (kwa mujibu wa taarifa za ndani) ila ikashindika sababu jaji alipata udhuru.

Lulu amekua chini ya ulinzi toka kifo cha mwigizaji staa wa movie Tanzania Steven Kanumba April 2012.

Vida ft Linex - Baba awena ( Video )


LULU KUPATA DHAMANA KESHO



Taarifa za uhakika nilizozipata kwa sasa ni kwamba kuna uwezekano mkubwa mwigizaji Lulu akatoka kwa dhamana kesho Tarehe 25.

Uhakika wa Lulu kupata dhamana ulikua jana jumatano lakini ikawa imeshindikana kutokana na kuahirishwa kwa sababu jaji alipata dharura na pia kiwango cha pesa za dhamana kilikua hakijatimia.

Chanzo cha kuaminika kimesema dhamana ya kumtoa Lulu ambae amekua chini ya ulinzi kuanzia April 2012 ni milioni 20 za kitanzania.

Lulu amekua akishikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mwigizaji Steven Kanumba tangu April 2012, endelea kuipitia abrangula.com kwa stori zaidi.

NU Film: HUKUMU YANGU Kutoka kwa Dk. Chen


VIDEO: Keisha Ft. Diamond-Nimechoka

Ile picha iliyosambaa mtandaoni ikimuonyesha Diamond anajipaka poda ndani ya gari akiwa na msichana basi Script yake ilikuwa ya humu ndani, tizama video mpya ya Keisha akiwa na Diamonda track inaitwa nimechoka kupitia InfoGramme Blog.

Kuhusu Video hii Keysha amesema,  "Nimetumia zaidi ya shilingi za Tanzania Milioni 10 kuandaa video hii, hii ikiwa ni pamoja na malipo kwa AJ ambaye amesimamia kazi yote, video hii ilikuwa itoke muda mrefu lakini kutokana na msururu wa ratiba ya shoo za nje ya nchi nilijikuta mara kadhaa ninahirisha kushoot, nashukuru Mungu imekamilika na huu ni mwanzo wa mafanikio yangu katika mwaka huu wa 2013"

FID Q APEWA CHET MAALUM CHA HESHIMA KUTOKA UNDER THE SAME SUN

Fid Q akikabidhiwa cheti hicho na Mr. Peter Ash
Mkali wa mashairi na flow kutoka Mwanza Fareed Qubanda a.k.a Fid Q ametunukiwa cheti maalum cha shukurani na shirika linalosaidia watu wenye ulemavu wa ngozi(albino) linalojulikana ma "Under The Same Sun" kwa mchango wake mkubwa katika kusapoti kampeni ya shirika hilo.
 
Fid Q amepost picha akiwa na mwanzilishi na mwenyekiti wa shirika hilo la Canada, Peter Ash, na kuisindikiza picha hiyo na maandishi yanayosomeka.. "Just received CERTIFICATE OF APPRECIATION from the one and only Mr. Peter Ash (CEO of Under The Same Sun)."

Mwaka jana Fid Q akiwa na wasanii wengine wa muziki wa kizazi kipya na walizungukia mikoa ya kanda ya ziwa na kuwahamasisha watu kupinga mauaji ya albino wakiwa na shirika hilo.

MBEYA FM na PRECISION AIR

Jiandae kuwa Mmoja ya watakaotumia Vyema Dakika 90 Bora., Mbeya FM inakupa nafasi ya kutumia Dakika 90 Bora kwa Usafiri bora na wa Uhakika wa Anga kwa kutumia Precision Air..!!#Tafadhali sikiliza 89.5 Mhz Mbeya FM muda wote uwe moja ya Washindi.#Team-Mbeya FM#

TABASAMU: Infogramme na Abby


Mtoto katoka shuleni huku analia, alipofika nyumbani. Baba yake akamuuliza ''unalia nini'? MTOTO '' Nimepigwa na mwalimu na nimeambiwa twende wote shuleni''. Wakaenda shuleni na wakaingia ofisini. MWALIMU ''Karibuni, mtoto wako tumemuuliza Nairobi iko wapi kashindwa, ndio maana tumemchapa'' Baba akamgeukia mtoto wake na kumpiga vibao, akamwambia ''mpumbavu mkubwa, kila siku nakukataza kuchezea vitu vya watu hukomi, haya NAIROBI ya mwalimu umepeleka wapi'?

Mbeya: BIBI MBARONI NA LITA 9 ZA GONGO ni muuzaji kitamboo



Mfano: Uandaaji wa Gongo
Jeshi la polisi mkoani Mbeya linamshikilia Bibi wa miaka 62, Marry Mbuya mkazi wa Kabwe jijini Mbeya kwa tuhuma za uuzaji wa pombe haramu  (Gongo).

Polisi wakiwa katika doria walimkamata mtuhumiwa nakiwa na lita 9 za pombe hiyo ya moshi jana asubuhi akiwa maeneo ya Mwanjelwa na jitihada za kumfikisha mahakamani zinaendelea.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Diwani Athumani, amethibitisha tukio hilo na kuwaasa watu kuachana na matutumizi ya pombe hiyo kwani ni kinyume na sheria pia hatari kwa afya zao.

IZZO B: Ball Player kwa hewa

Mchonvu          Izzo B                Dozen
Uzinduzini na team Clouds Intertainment
Izzo na Quick
Hii ndio Picha ya Cover ya Track hiyo.
Huu ndio uzinduzi wa track ya Izzo B aliyomshirikisha QuickRocka na Mangwair iitwayo Ball Player ambayo imeachiwa rasmi Jumatano ya leo..  Fuata link hii kuiskiliza na kudownload..  Bofya HAPA (By Infogramme Blog)

NU Video: Hemedy PHD - Going crazy

ALISREMA ITATOKA VALENTINE DAY
Hemedy Suleiman baada ya kuachia ngoma yake mpya mwaka jana inayokwenda kwa jina la Going Crazy kutoka B hits alisema anatarajia kuachia video yake siku ya Valentine day lakini leo ipo hewani. Tizama Video hiyo kwa kubofya hapo katikati..

COMMING SOON: Izzo B Feat. Ngwair, QuickRocka - Ball Player, JumaTano Hii

Izzo B amesema kuwa Juma tano hii anaachia ngoma yake ya kwanza kwa mwaka 2013 iitwayo Ball Player ambayo amemshirikisha Mangwair na Quick Rocka, Ngoma hiyo imetengenezwa na Nahreel na Lamar.
Cover ya track hiyo iliyotupiwa na Ngwair ktk Twitter
Stay tuned kucheck Izzo anauanza mwaka vip?

SKILIZA & DOWNLOAD MIXING ZA DJ SPEED wa HighLands FM Radio HAPA