DUNIA NZIMA MTU MMOJA ANAKOSA CHAKULA KATI YA WATU 8

Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limetangaza kuwa  zaidi ya asilimia 12 ya jamii ya watu duniani,  wanakabiliwa na njaa.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Jose Silva, ameeleza kuwa, kutokana na wastani huo, ina maana kwamba mtu mmoja kati yawatu 8 ana tatizo la ukosefu wa chakula.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa, watu milioni 840 wanakabiliwa na ukosefu wa chakula kwa mwaka huu ambapo idadi hiyo imepungua kutoka watu milioni 870 kwa mwaka jana.

Hayo yamesemwa katika mkutano wa Siku ya Kimataifa ya Chakula uliofanyika katika Wizara ya Jihadi ya Kilimo ya nchini Iran.

No comments:

Post a Comment

SKILIZA & DOWNLOAD MIXING ZA DJ SPEED wa HighLands FM Radio HAPA