LYK Movie: Kituo cha kijeshi Marekani chavamiwa, wanne wauawa


Habari kutoka Washington zinasema kuwa watu 4 wameuawa na wengine 8 kujeruhiwa baada ya mtu asiyejulikana kuvamia makao makuu ya jeshi la wanamaji mjini Washington na kuanza kufyatua risasi.

Habari zaidi zinasema kuwa mtu huyo bado hajapatikana ingawa inaaminika bado yuko katika jengo hilo.

Wakuu wa kituo hicho cha kijeshi wanasema maafisa kadhaa wamepigwa risasi na mvamizi huyo.
Polisi zaidi wamepelekwa kwenye eneo hilo huku shughuli katika uwanja wa ndege wa Reagan ulioko karibu zikisitishwa kwa muda.

Zaidi ya wafanyakazi 3000 wanafanya kazi katika kituo hicho kilichovamiwa. Kitengo hicho kijulikanacho kama Naval Sea Systems Command ndicho kinachohusika na utengenezaji, ukarabati au ununuzi wa meli za kijeshi pamoja na nyambizi za jeshi la Marekani.

Haijabainika ni vipi mtu huyo aliweza kuingia katika eneo hilo lenye ulinzi mkali.

No comments:

Post a Comment

SKILIZA & DOWNLOAD MIXING ZA DJ SPEED wa HighLands FM Radio HAPA