NIMEPEWA NA MASANJA HII

Jamaa mmoja msomi msomi kapanda bus toka Dar anakwenda Mwanza. Kwenye siti akakuta mtoto mdogo wa miaka kama 9 hivi. Kwa kuwa jamaa anajiona msomi na anapenda kudadisi akili za wengine akaona ni bora safari ikiwa inaendelea alete mada wajadili na dogo. Akaanza: Dogo hujambo? Naona unasafiri mwenyewe. Naitwa Mayala, na mimi nakwenda Mwanza. Naomba tupige stori. Unajua safari na stori ndo inaenda vizuri. Dogo akamcheki halafu akamjibu: Poa, naenda Mwanza pia. Naitwa Chale. Anza wewe stori. Jamaa akaanza: Hebu tujadili uwepo wa Mungu, hivi wewe unadhani Mungu yupo au ni stori tu? Dogo akakaa kimya kwa muda halafu akajibu: Mimi naona kabla ya kuanza kujadili hivyo, hebu tujadili hili kwanza: unawajua ng'ombe na mbuzi? Wote wanakula majani lakini vinyesi vyao ni tofauti. Kwa nini? Jamaa msomi akatafakari kwa muda halafu akajibu: Hiyo siyo fani niliyosomea. Ila sijui kwa nini. Dogo akamjibu: Sasa kama huwezi hata mjadala unaohusu vinyesi, utawezaje kujadili kitu kikubwa kama uwepo wa Mungu?

No comments:

Post a Comment

SKILIZA & DOWNLOAD MIXING ZA DJ SPEED wa HighLands FM Radio HAPA